Habari ya saizi wananchi wenzangu.Mimi ni mwanaume nina miaka 27 ni mkazi wa arusha,mnamo mwaka 2011 nilikutana na msichana (Ambaye ndio mchumba wangu),ilipofika mwaka 2013 tukabahatika kupata mtoto wa kiume.Sasa wazazi wa mwanamke hawataki mimi niishi na mtoto wao kwa sababu ya tofauti zetu za kidini,na mchumba wangu yeye anasema yuko tayari hata kubadili dini kwa ajiri yangu tatizo ni wazazi wake,na inafika mahali ndgu zake wananiombea mabaya ilimradi niachane na mtoto wao,sasa nimekuja kwenye ukurasa huu wa ushauri wako kuomba msaada wa mawazo mana imeshakuwa tatizo.